Wanawake nchini Venezuela wanatumia kemikali haramu
kuongeza ukubwa wa makalioyao na kujiletea madhara makubwa ya kiafya Hii
ni kutokana na mtindo ambao unaonekana na wengi nchini humo kwamba
mwanamke mwenye makalio makubwa ndiye anayependeza zaidi
Wataalam wa magonjwa ya kina mama na watoto
wamebainisha madhara ambayo yanaweza kuwapata kina mama na wasichana
wenye tabia ya kuvaa nguo za ndani wakati wa kulala, maumbile ya kike
yanaitaji kupumua ili kuzuia maambukizi kama vile fangasi ndio maana madaktari wanashauri kulala bila nguo au kuvaa vinguo vyepesi..
Habari njema ni kwamba kuna uwezekano wa Janga la Ukimwi kudhibitiwa
ifikapo mwaka 2030, kwa mujibu wa ripoti ya shirika la Umoja wa mataifa
la kupambana na Ukimwi.
Shirika la afya duniani, limewaasa wanaume wanaoshiriki mapenzi ya
jinsia moja, kutumia dawa za kupunguza makali ya HIV hata ikiwa
hawajaambukizwa HIV.
Kuna sababu mbalimbali zinazoweza kumfanya mtu asishike mimba. Sababu
hizo zinaweza zikawa zinamhusu mwanamke, mwanamume au wakati mwingine
kutojulikana kabisa hali hiyo imesababishwa na nini. Wataalamu wanasema
kwamba kwa miaka 20 iliyopita matatizo yanayohusu kushindwa kuzaa
yameongezeka kwa kiwango kikubwa na asilimia 25 ya watu wanaotaka kubeba
mimba na kuzaa mtoto wanakabiliwa na tatizo hilo.